HIVI karibuni Rais wa Kenya, Mheshimiwa Uhuru Kenyatta alikuwa ziaraniUchina na katika mikataba aliyosaini ni pamoja na ule wa ujenzi wa reli toka Malabo hadi Mombasa, hii ikiwa na maana Uganda haina tenampango wa kupitisha mizigo yake huko Tanga.
Chokochoko zetu na Rwanda na Malawi kwa kiasi fulani zinazikimbiza nchihizo kuing’ang’ania Kenya au Msumbiji, kama njia yao kuu ya usafirishaji na siyo Tanzania.
Siasa zisizoangalia maslahi ya nchi na watu wake, binafsi, ninaamini siyo siasa zenye mwelekeo sahihi. Baadhi ya misimamo na mitazamo tuliyoichukua ingelifaa ipitiwe upya na sisi wenyewe kujirudi kwa kuangalia masilahi ya muda mrefu ya nchi na watu wake. Tanzania ni nchi kubwa, lakini isitumie ukubwa wake kuwafanya wengine kujiona wadogo na watu wasiyo na thamani.
Tukifanya hivyo, tutakuwa na kazi kubwa ya kuwa na marafiki wa kweli miongoni mwa nchi jirani zinazotuzunguka. Siyo vyema wanasiasa wetu pia kukurupuka na kuingiia mambo ya kidiplomasia.
Tungewaachia wanadiplomasia wao wenyewe waifanye kazi waliyoisema na wanayoijua.
Hatuwezi kuilaumu Kenya kwa kutaka kuiokoa bandari yake ya Mombasa na vilevile hatuwezi kugombana nao kuhusu uamuzi wao wa kujenga bandari mpya kule Lamu.
Share To:
Magpress

MagPress

Vestibulum bibendum felis sit amet dolor auctor molestie. In dignissim eget nibh id dapibus. Fusce et suscipit orci. Aliquam sit amet urna lorem. Duis eu imperdiet nunc, non imperdiet libero.

0 comments so far,add yours