HIVI karibuni Rais wa Kenya, Mheshimiwa Uhuru Kenyatta alikuwa 
ziaraniUchina na katika mikataba aliyosaini ni pamoja na ule wa ujenzi 
wa reli toka Malabo hadi Mombasa, hii ikiwa na maana Uganda haina 
tenampango wa kupitisha mizigo yake huko Tanga.
Chokochoko zetu na Rwanda na Malawi kwa kiasi 
fulani zinazikimbiza nchihizo kuing’ang’ania Kenya au Msumbiji, kama 
njia yao kuu ya usafirishaji na siyo Tanzania.
Siasa zisizoangalia maslahi ya nchi na watu wake, 
binafsi, ninaamini siyo siasa zenye mwelekeo sahihi. Baadhi ya misimamo 
na mitazamo tuliyoichukua ingelifaa ipitiwe upya na sisi wenyewe 
kujirudi kwa kuangalia masilahi ya muda mrefu ya nchi na watu wake. 
Tanzania ni nchi kubwa, lakini isitumie ukubwa wake kuwafanya wengine 
kujiona wadogo na watu wasiyo na thamani.
Tukifanya hivyo, tutakuwa na kazi kubwa ya kuwa na
 marafiki wa kweli miongoni mwa nchi jirani zinazotuzunguka. Siyo vyema 
wanasiasa wetu pia kukurupuka na kuingiia mambo ya kidiplomasia.
Tungewaachia wanadiplomasia wao wenyewe waifanye kazi waliyoisema na wanayoijua.
Hatuwezi kuilaumu Kenya kwa kutaka kuiokoa bandari
 yake ya Mombasa na vilevile hatuwezi kugombana nao kuhusu uamuzi wao wa
 kujenga bandari mpya kule Lamu.

0 comments so far,add yours