KOCHA wa Shakhtar Donetsk ya Ukraine Mircea Lucescu amesema kuwa klabu yake imeikataa ofa ya pauni milioni 25 kutoka kwa Chelsea kwa ajili ya kumsajili kiungo mshambuliaji William.

Kiungo huyo raia wa Brazili amekuwa akiwindwa na Chelsea toka mwezi Januari, na kocha wake amewahi kukiri kuwa watamruhusu kuondoka kwa bei sahihi.

"Nimemwambia William kuwa anaweza kuondoka lakini kama tutapokea ofa sahihi. Willium ni mchezaji mzuri sana." Alisema Lucescu.

Lucescu alienda mbali zaidi kwa kusema kuwa William ni mchezaji mzuri zaidi ya Hazard na kuhoji iweje Chelsea itoe pesa nyingi kwa ajili ya Hazard lakini itoe pesa ndogo kwa ajili ya Willium wakati William ni bora zaidi ya Hazard.

"Waliilipa Lille pesa nyingi kwa ajili ya Hazard lakini hawapo tayari kulipa pesa nyingi kwa ajili ya William ambaye kwangu mimi ni bora zaidi ya Hazard." Alisema kocha huyo.
Share To:
Magpress

MagPress

Vestibulum bibendum felis sit amet dolor auctor molestie. In dignissim eget nibh id dapibus. Fusce et suscipit orci. Aliquam sit amet urna lorem. Duis eu imperdiet nunc, non imperdiet libero.

0 comments so far,add yours