Wagonjwa wanaohitaji rufaa ya matibabu ya dharura kutoka katika vijiji mbalimbali vya kata za nyanguge, Kisesa na Lugeye wilayani Magu, wako kwenye hatari ya kupoteza maisha yao kufuatia mgomo wa madereva wa magari ya kubeba wagonjwa unaoendelea endapo hatua za haraka hazitachukuliwa na uongozi wa halmashauri ya wilaya hiyo kuwalipa fedha zao za uhamisho kiasi cha shilingi milioni tano.
Madereva wa magari ya wagonjwa waliogoma kuhamia kwenye vituo vyao vipya ni Andrew Kitalagwa, aliyehamishiwa kituo cha afya Nyanguge, Mohamed Bakari aliyehamishiwa Kisesa na Jackson Saguda ambaye amepangiwa kazi  katika kituo cha afya Lugeye, madereva hao walihamishiwa kwenye vituo hivyo tangu machi 19 mwaka huu lakini hadi sasa bado hawajaripoti kazini, jambo ambalo limewasikitisha madiwani wa halmashauri ya wilaya hiyo.
 
Kaimu mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Magu Yesse Kanyuma akizungumza katika kikao cha baraza la madiwani wa halmashauri ya wilaya hiyo amewataka madereva hao kurudi kazini mara moja wakati madai yao yakiendelea kushughulikiwa ili kuokoa maisha ya wagonjwa wanaoteseka kwa kukosa matibabu ya dharura.
Share To:
Magpress

MagPress

Vestibulum bibendum felis sit amet dolor auctor molestie. In dignissim eget nibh id dapibus. Fusce et suscipit orci. Aliquam sit amet urna lorem. Duis eu imperdiet nunc, non imperdiet libero.

0 comments so far,add yours