Watu wawili wanashikiliwa na jeshi la polisi mkoa wa Morogoro baada ya kupatikana na lita 30 za mafuta ya transfoma baada yakukata nguzo za umeme kuvunja transfoma na kuiba mafuta na kusababisha wakazi wa eneo la kola mjini Morogoro kukosa huduma ya umeme kwa muda mrefu.
Kamanda wa polisi mkoa wa Morogoro Leonard Paul amethibitisha kukamatwa kwa watu hao ambapo amesema watuhumiwa   walikamatwa katika eneo la kola kwa kamnyonge manispaa ya Morogoro wakihujumu miundombinu ya umeme ikiwemo kuiba mafuta ya trasfoma na kukata nguzo za umeme ambapo jeshi la polisi linaendelea kuwahoji watu hao na mara baada ya upelelezi kukamilika watafikishwa mahakamani.
 
Naye afisa uhusiano wa shilika na umeme Tanesco mkoa wa Morogoro Ester Msaki amsema mafuta hayo yana thamini ya zaidi ya shilingi laki tatu ambapo amewataka wananchi kuendelea kuwa na ushirikiano kwa kuwafichua wanaohujumu miundombinu ya umeme kwani shirika linaendelea kupata hasara na kusababisha baadhi ya wananchi kukosa huduma ya umeme.
 
Kwa upande wao wakazi wa manispaa ya Morogoro wameiomba serikali kuongeza ulinzi na kuwachukilia hatua kali watakaobainika wakihujumu miundombinu ya umeme na kusababisha wananchi kuishi gizani kwakukosa huduma ya umeme.

Share To:
Magpress

MagPress

Vestibulum bibendum felis sit amet dolor auctor molestie. In dignissim eget nibh id dapibus. Fusce et suscipit orci. Aliquam sit amet urna lorem. Duis eu imperdiet nunc, non imperdiet libero.

0 comments so far,add yours