Moto mkubwa uliotokozea wakati wa jioni umeteketeza kabisa moja kati 
ya nyumba mbili za mfanyabiashara maarufu wa Zanzibar Naushad Mohamed na
 kusababisha hasara ya mamilioni ya fedha.
Moto huo uliutokozea eneo la Beitras Njekidogo ya 
mjini Zanzibar ulianza wakati wa saa kumi jioni lakini pamoja na kikosi 
cha zimamoto kufika kwa mudamfupi upepo mkali uliokuwa ukivuma 
ulisababisha moto huo kuwa na kasi na kuweza kutekekteza nyumba hiyo 
huku taarifa ya familia ikielezea chanzo cha moto huo umetokana na 
hitilafu ya umeme.
Wakizungumza na ITV mmiliki wa nyumba hiyo Bw 
Naushand Mohamed mohamec amesema moto huo ulikuja ghafla na yeye alikuwa
 katika nyumba nyingine huku aksiema moto huo umeangamiza hati zake zote
 za nyumba na nyingine za biashara huku mkuu wa opresheni wa kikosi cha 
zima moto sasa wa zimamoto Suleiman amesema moto huo ulikuwa mkubwa.
Moto huo ulizua mtafaruku mkubwa huku umati wa watu
 kujazana nje ya jengo hali iliyosababisha jeshi la polisi kuweka ulinzi
 mkubwa ambapo polisi walilazimika kulinda nyumba hiyo ndani na nje 
wakiwa na silaha.
0 comments so far,add yours