
Baadhi ya wananchi wa eneo la Mloganzira Kwembe jijini Dar es Salaam wamevamia ofisi za wizara ya ardhi nyumba na maendeleo ya makazi wakishinikiza kulipwa madai yao ya fidia baada ya kupisha mradi wa chuo cha muhimbili na kusababisha shughuli za wizara hiyo kusimama kwa muda.
Wananchi hao wamevamia ofisi hizo huku wakiimba nyimbo mbalimbali 
zilizokuwa zikishinikiza kulipwa madai yao ambapo wamedai kuwa tangu 
waondoke kwenye maeneo yao kupisha mradi ni zaidi ya miaka kumi 
hawajalipwa licha ya Rais kuwaahidi kuwa hawataachwa bila kulipwa.
Kufuatia hali hiyo naibu waziri wa wizara hiyo Mh. Anjela Kairuki 
amelazimika kutoka ofisini na kuzungumza na wananchi hao ambapo 
amekutana na wakati mgumu kwani kila alipotaka kuzungumza nao baadhi yao
 walionekana kutoridhishwa na majibu yake na kuanza kumzomea, na baade 
aliweza kuwatuliza kwa kuwaeleza kuwa ndani ya siku saba watakwenda eneo
 husika kuzungumza nao.
Hata hivyo licha ya Mh.Kairuki kutoa kauli hiyo baadhi ya wananchi 
wamemweleza kuwa wakati wanamsubiri wanarudi kwenye maeneo yao huku 
wakitishia kusimamisha mradi hadi watakapolipwa fedha zao, ambapo 
kutokana na hali hiyo polisi walionekana kutanda katika eneo la wizara 
ya hiyo huku wengine wakiwa na silaha za moto.

0 comments so far,add yours