Chama cha demokrasia na maendeleo ( CHADEMA ), kimesema hakuna sababu ya wananchi wa kabila la wasukuma katika mikoa ya Shinyanga na Simiyu kuendelea kuwa maskini, wakati almasi peke yake iliyoanza kuchimbwa tangu mwaka 1942 katika mgodi wa mwadui, ingeweza kuboresha maisha yao mbali na wingi wa mifugo pamoja na uzalishaji wa zao la pamba na kusema wakati umefika kwa wananchi wa kabila hilo kutumia raslimali walizonazo katika kupiga vita umaskini.
Akihutubia mkutano wa hadhara katika uwanja wa lagangabilili wilayani itilima, mwenyekiti wa taifa wa chadema Mh. Freeman Mbowe amesema kwamba licha ya mikoa ya usukumani kusifika kwa uzalishaji wa pamba iliyopelekea kujengwa kwa viwanda vitano vya nguo ambavyo ni pamoja na Mwatex,Mutex,Kilitex,Kunguratex na urafiki wakati wa enzi za mwalimu Julius Nyerere, lakini amedai kuwa bado wasukuma ni maskini ukilinganisha na makabila mengine nchini kwa miaka 53 baada ya uhuru.
Mh. Mbowe ambaye pia ni kiongozi wa kambi rasmi ya upinzani bungeni akizungumzia mpango wa Chadema unaojulikana kama ‘FTP 200’ unaokusudia kuwafanya vijana wa kitanzania kuwa wazalendo kwa nchi yao katika kuwaepusha na vikundi vya kihalifu kama vile panya Road na Mbwa Mwitu kwa kusaidiana na jeshi la polisi kufichua vitendo vya uhalifu,amesema pindi ukikamilika mwezi juni mwaka huu utawafikia vijana zaidi ya milioni moja nchi nzima ambao wanaishi bila ajira rasmi kupata stadi za ujasiriamali,Elimu ya afya,nidhamu na kupiga vita Rushwa katika jamii.
Katika hatua nyingine wazee wa kabila la kisukuma wilayani humo wamemsimika mwenyekiti huyo wa taifa Chadema na mbunge wa jimbo la hai Mh.Freeman Mbowe kuwa Chifu wa kabila hilo baada ya kumvisha mgolole pamoja na kumkabidhi mkuki, ngao na kibuyu – huku wazee hao wakimpatia jina la mayengo na kutaka vyombo vya dola kutenda haki kwa vyama vyote vitakavyoshiriki katika uchaguzi mkuu.
Share To:
Magpress

MagPress

Vestibulum bibendum felis sit amet dolor auctor molestie. In dignissim eget nibh id dapibus. Fusce et suscipit orci. Aliquam sit amet urna lorem. Duis eu imperdiet nunc, non imperdiet libero.

0 comments so far,add yours