
Wananchi wa kata ya Nyankende katika 
wilaya ya kahama mkoani Shinyanga wameitaka serikali kutafuta mbinu za 
kupandisha bei ya pamba zao ambalo linategemewa katika shughuli zote za 
kimaendeleo hali  inayotishia kuporomoka kwa uchumi katika mkoa wa 
shinyanga na kuwafanya wananchi kuishi maisha duni na ya dhiki.
 
 
Hayo yamesemwa na diwani wa kata ya Nyankende wilayani kahama Mh. 
Doa Limbu kwa niaba ya wananchi wa kata hiyo katika mkutano wa hadhara 
ulioitishwa na mkuu wa mkoa wa shinyanga ili kujadili changamoto 
zinazowakabili wananchi hao ambapo kata hiyo haijawahi kutembelewa na 
mkuu wa mkoa yeyote tangu ianzishwe.
Naye mkuu wa wilaya ya kahama Bw.Benson Mwampesya amewataka 
wananchi wa kata ya Nyankende kulima mazao mengine ya biashara na 
chakula ikiwemo zao la alizeti kwakuwa kuanguka kwa bei ya zao la pamba 
sio swala la tanzania pekee na hakuna namna ya kupandisha bei ya zao 
hilo kwa haraka.
Kwa upande wake mkuu wa mkoa wa shinyanga Bw.Ally Nasoro Rufunga 
amewaahidi wananchi hao kuwaletea wawekezaji watakaoingia ubia katika 
kilimo cha mkataba hali itakayosababisha kukua kwa sekta ya kilimo 
katika kata hiyo.

0 comments so far,add yours