Rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Dk Jakaya Mrisho Kikwete amefanya mabadiliko ya wakuu wa wilaya ambapo amewateua wakuu wa wilaya 27 wapya na 64 kuhamishwa kwenye vituo vyao vya awali huku akitengua uteuzi wa wakuu 12 na wengine 7 kupangiwa majukumu mengine na waliobaki 42 wakisalia kwenye vituo vyao vya sasa.
Akitoa taarifa ya mabadiliko hayo kwa niaba ya rais waziri mkuu wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Mhe Mizengo Pinda amesema katika nafasi 27 ambazo wameteuliwa wakuu wa wilaya wapya zimetokana na sababu mbalimbali ikiwemo kufariki dunia kwa wakuu wa wilaya watatu, kupandishwa kwa wakuu watano kuwa wakuu wa mikoa, saba kupewa majukumu mengine ambapo hapa anataja baadhi ya majina ya wakuu walioteuliwa huku kukiwa na sura nyingi mpya za vijana.
 
Waziri mkuu pia akataja majina ya wakuu wa wilaya 12 ambao uteuzi wao umetenguliwa na rais kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo umri na matatizo ya kiafya ambapo miongoni mwa majina mashuhuri ni pamoja aliyekuwa mkuu wa wilaya ya kiteto martha umbula, james ole Millya Longido na Elibariki Emmanuel Kingu aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Igunga.
 
Mhe waziri mkuu amebainisha kuwa mabadiliko hayo yanaanza kazi mara moja huku wakuu wapya 27 wakipatiwa semina maalum ya uongozi na namna ya kutekeleza majukumu yao itakayotolewa na ofisi ya waziri mkuu tawala za mikoa na serikali za mitaa.

Share To:
Magpress

MagPress

Vestibulum bibendum felis sit amet dolor auctor molestie. In dignissim eget nibh id dapibus. Fusce et suscipit orci. Aliquam sit amet urna lorem. Duis eu imperdiet nunc, non imperdiet libero.

0 comments so far,add yours