Mkuu wa mkoa wa tabora BW. RUDOVICK mwananzira, amesema vifo vya 
akinamama na watoto vinaweza kuzuilika, kama kila mmoja atatimiza wajibu
 wake, ambapo  amemuagiza mganga mkuu wa mkoa huo kuvitolea maelezo vifo
 hivyo kutokana na kupanda na kushuka kila mwaka na  atabainika 
aliyehusika hatua zichukuliwe dhidi yake.
Bw. Rudovick Mwananzira anetoa kauri hiyo wakati akizungumza na 
wadau wa afya mkoani Tabora, katika akizindua mpango mkakati wa 
kupunguza vifo vya akinamama na watoto, pamoja na kutathimini maendeleo 
ya kupunguza vifo hivyo ambapo amebainisha kushindwa kufikia lengo la 
chini ya vifo theruthi mbili  mwaka 2015,
Aidha amesema kuwa, lengo lililowekwa la kupunguza vifo  kutoka 
112/100,000, kufikia 90/100,000, mwaka 2013, halikufikiwa na matokeo ya 
 vikaongezeka mpaka 117,/100,000, 2014, na hivyo unahitajika uwajibikaji
 ili kufikia lengo lililokusudiwa, na hatua za makusudi zichukuliwe 
ikiwemo kuwajibishana.

0 comments so far,add yours