Mkuu wa mkoa wa tabora BW. RUDOVICK mwananzira, amesema vifo vya akinamama na watoto vinaweza kuzuilika, kama kila mmoja atatimiza wajibu wake, ambapo  amemuagiza mganga mkuu wa mkoa huo kuvitolea maelezo vifo hivyo kutokana na kupanda na kushuka kila mwaka na  atabainika aliyehusika hatua zichukuliwe dhidi yake.
Bw. Rudovick Mwananzira anetoa kauri hiyo wakati akizungumza na wadau wa afya mkoani Tabora, katika akizindua mpango mkakati wa kupunguza vifo vya akinamama na watoto, pamoja na kutathimini maendeleo ya kupunguza vifo hivyo ambapo amebainisha kushindwa kufikia lengo la chini ya vifo theruthi mbili  mwaka 2015,
 
Aidha amesema kuwa, lengo lililowekwa la kupunguza vifo  kutoka 112/100,000, kufikia 90/100,000, mwaka 2013, halikufikiwa na matokeo ya  vikaongezeka mpaka 117,/100,000, 2014, na hivyo unahitajika uwajibikaji ili kufikia lengo lililokusudiwa, na hatua za makusudi zichukuliwe ikiwemo kuwajibishana.
 
Awali katibu tawala wa mkoa wa Tabora Bibi Kudra Mwinyimvua akimkaribisha mkuu wa mkoa katika uzinduzi huo, amesema kuwa uwepo wa mashirika binafsi na taasisi za dini zinayojihusisha na kupunguza vifo vya akinamama ni msaada kwa serikali mkoani, ambapo ratibu wa vifo vya akinamama na watoto kanda ya magharibi Bibi Mather Ndimbo akiwataka jamii nzima kuguswa na changamoto hiyo
Share To:
Magpress

MagPress

Vestibulum bibendum felis sit amet dolor auctor molestie. In dignissim eget nibh id dapibus. Fusce et suscipit orci. Aliquam sit amet urna lorem. Duis eu imperdiet nunc, non imperdiet libero.

0 comments so far,add yours