Mwenyekiti Mtendaji wa IPP Dr. Reginald Mengi amesema iwapo serikali 
itaandaa mazingira mazuri vijana na Watanzania kwa ujumla wanaweza 
kujikwamua kiuchumi kwa kutumia akili, juhudi,  na utajiri wa raslimali 
za taifa.
Mwenyekiti Mtendaji wa IPP DR Reginald Mengi ameyasema hayo jijini 
Dar es salaam wakati akizindua shindano jipya la kubuni Wazo la Biashara
 litakaloendeshwa kwa miezi sita mfululizo kuanzia Januari 2015, na kila
 mwezi mshindi mmoja atajishindia zawadi ya shilingi milioni 10 
atakazozitumia kama mtaji wa kutekelezea kwa vitendo wazo lake la 
biashara.
Amesema Shindano hilo linalojulikana kama 3N ikiwa ni kifupisho cha
 ‘NITABUNI biashara, NITATEKELEZA na NITAFANIKIWA’, litawashirikisha 
Watanzania pekee na litaendeshwa kwa njia ya mtandao wa kompyuta ambapo 
mshiriki anatakiwa atatume wazo lake kwa anuani ya twita @regmengi 
shindano la wazo la biashara.
Katika kupata mshindi, jopo maalum la wataalamu watapitia mawazo 
yatakayowasilishwa na kuteua mawazo 10 bora, na watunzi wa mawazo hayo 
10 watafanyiwa usaili kwa njia ya simu ili jopo lijiridhishe kuwa mawazo
 waliyotoa ni yao binafsi na jinsi walivyojiandaa kuyatekeleza 
kibiashara. Jopo la wataalamu litamteua mshindi baada ya usaili huo.

0 comments so far,add yours