Wananchi wa kata ya  msanga mkuu wilaya ya mtwara vijijini wamelazimika kurudia usafiri wa mitumbwi baada ya kivuko kilicholetwa  na serikali miezi miwili iliyopita kusitisha safari zake baada ya  kugonga mwamba na kuvunja gia.
Akizungumzia tatizo hilo kaimu meneja wa wakala wa ufundi na umeme tamesa mkoa wa mtwara Elitraudi Mmbemba  amesema tatizoli hilo limetokana na upepo mkali na hivyo nahodha kukosa mwelekeo na kugonga mwamba.
 
Hata  hivyo amesema hakuna abiria aliyepata tatizo kuhusiana na tukio hilo na tayari kifaa hicho kimemepatikana  jijini Dar es salaam na wakati wowote kitawasili na kufungwa ili kiendelee na kazi kama kawaida.
 
Wakizungumzia adha  ya kurudia usafiri wa mitumbwi  baadhi ya wananchi wa msanga mkuu ambao sehemu kubwa ya maitaji  huyapata mtwara mjini wamesema kifaa hicho kiharakishwe mapema kufungwa kusudi waandelee na usafiri wao kama kawaida kuliko wanaoutumia wa mtumbwi ambao hauaminiki asilimia kubwa. 
 
kivuko hicho hutumia muda wa dakika 15 kuvusha watu kutoka gati ya mtwara kuelekea ghati ya msanga mkuu.

Share To:
Magpress

MagPress

Vestibulum bibendum felis sit amet dolor auctor molestie. In dignissim eget nibh id dapibus. Fusce et suscipit orci. Aliquam sit amet urna lorem. Duis eu imperdiet nunc, non imperdiet libero.

0 comments so far,add yours