Kuelekea mwishoni mwa mwaka huwa kila mtu ana utaratibu wake wa kumaliza mwaka.Hivi ndivyo Madam Rita kutoka kampuni ya Benchmark Production ameamua kuufunga mwaka huu.


Madam Rita kupitia akaunti yake ya Facebook amekuwa akitoa stori mbalimbali zinazomuhusu juu ya mambo mengi ambayo yamewahi kumtokea/ kumpata kipindi cha nyuma au katika maisha yake kiujumla.
Moja ya vitu hivyo ni suala ya yeye kupata mimba katika umri mdogo ambalo ameamua kuliweka wazi kwenye ukurasa wake wa FB kama hivi…

Huu ndio ujumbe wake alioupost '

Jambo mmoja msilofahamu kuhusu mimi....
Nilipata ujauzito nikiwa na umri mdogo sana. Kwa jamii yetu inayotuzunguka, ukizaa katika umri mdogo, watu huwa wanakunyanyapaa, hukuona haufai kuwa katika jamii na hata kukuhukumu. Kwa umri ule niliona ni kama hamna tena maisha kwangu lakini sikukata tamaa na leo hii ujasiri wangu na kitu kinachonipa msukumo wa maisha hadi kufika hapa nilipo ni hicho kilichonikuta nikiwa na umri mdogo.
"Kukataa tamaa isiwe ndio chaguo lako la kwanza'Aliandika Madam Rita.
Share To:
Magpress

MagPress

Vestibulum bibendum felis sit amet dolor auctor molestie. In dignissim eget nibh id dapibus. Fusce et suscipit orci. Aliquam sit amet urna lorem. Duis eu imperdiet nunc, non imperdiet libero.

0 comments so far,add yours