LUSAKA, ZAMBIA
MAHAKAMA ya Katiba nchini Zambia imetupilia mbali kesi ya mgombea urais wa chama cha upinzani cha United Party for National Development (UPND), Hakainde Hichilema dhidi ya ushindi wa Rais Edgar Lungu.
Katika uamuzi wa wengi, jopo la majaji katika mahakama hiyo liliamua kuwa muda wa mwisho uliowekwa kusikiliza kesi hiyo ulikuwa umekwisha.
Lungu alitetea kiti chake baada ya kujipatia zaidi ya asilimia 50 ya kura katika uchaguzi uliofanyika Agosti 11, mwaka huu.
Lakini Hichilema alipinga matokeo hayo na kuwasilisha ombi la kuyapinga Agosti 19.
Sheria inasema mahakama ya kikatiba ina siku 14 kusikiliza kesi hiyo.
Lakini muda huo ulikumbwa na mabishano na ilipofika Ijumaa, mawakili wa Hichilema waliondoka mahakamani wakidai ukosefu wa muda.
Hivyo, mahakama hiyo iliendelea mapema jana na kutangaza uamuzi huo.
Share To:
Magpress

MagPress

Vestibulum bibendum felis sit amet dolor auctor molestie. In dignissim eget nibh id dapibus. Fusce et suscipit orci. Aliquam sit amet urna lorem. Duis eu imperdiet nunc, non imperdiet libero.

0 comments so far,add yours