Saa 10 jioni~atakua na press conference na waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na michezo Nape Nnauye Kempisk hotel.

Baada ya hapo msafara kuelekea Escape one utaanza kupitia mitaa ya Samora, clock tower, Mnazi mmoja, barabara ya Uhuru, Kamata, hadi karume.

Kisha barabara ya Kawawa kuanzia ofisi ya mkuu wa mkoa, kigogo, magomeni usalama, kinondoni, hadi morocco, na kuifuata barabara ya Ally Hassan mwinyi kupitia Victoria, Makumbusho, Sayansi, Bamaga hadi Mwenge.

Msafara huo utazungukia Kawe, Lugalo, mlalakuwa na kumalizikia Escape one ambapo wanamichezo na wasanii mbalimbalo watapata nafasi ya kupiga nae picha na kumpongeza.

Watu wote wanaombwa kujitokeza barabara sehemu ambazo msafara wa shujaa Mbwana Ally Samatta utapita.

Share To:
Magpress

MagPress

Vestibulum bibendum felis sit amet dolor auctor molestie. In dignissim eget nibh id dapibus. Fusce et suscipit orci. Aliquam sit amet urna lorem. Duis eu imperdiet nunc, non imperdiet libero.

0 comments so far,add yours