Baadhi ya waathirika wa mafuliko katika kijiji cha mwakata wilaya ya kahama mkoani shinyanga wameladhimika kuifunga barabara ya isaka kahama na kuathiri kwa muda mawasiliano katika nchi ya rwanda,burundi na uganda wakishinikiza serikali kuwagawia chakula,magodoro,branketi.mahema na shuka baada ya kunyeshewa na mvua usiku wakati vifaa vya misaada vikiwa vimefungiwa kwenye magara hali iliyosababisha jeshi la polisi kuwatawa na wananchi kwa mabomu ya machozi na kufungua njia ili gari ziendelee na safari.
Vurugu hizo  zimedumu saa moja ambapo kundi la wananchi wenye hasila wakiillamika kamati ya maafa kwa kushindwa kuwahudumia waathirika kwa wakati hali iliyosababisha waathirika wanaolala nje kunyeshewa mvua huku wakinamama wakila ani nguvu kubwa iliyoumika kutuliza ghasia zilizosababisha watoto kupotea kutokana na mabomu ya machozi yaliyotumika kutawanya wananchi waliofunga barabara.
 
Kufuatia vurugu hizo mbunge wa jimbo la msalala Mh.Ezekiel Maige ameladhimika kufika kwenye eneo la tukio na kujionea hali halisi ambapo amewasihi wananchi kuwa watulivu wakati akifanya mipango ya kuzungumza na kamati ya maafa ili iweze kutoa vifaa vinavyolalamikiwa na vigawiwekwa walengwa.
 
Alipotakiwa kujibu malalamiko hayo katibu wa maafa wilaya ya kahama ambaye ni mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya ushetu kahama Bi.Isabela Chilumba amesema vurugu hizo zinasababishwa na wanasiasa na kwamba kamati ya maafa imeba ini kunakundi la vijana kutoka  vijiji jirani wakivizia chakula na vifaa vya misaada.
 
Naye  mkuu wa mkoa wa shinyanga Bw.Ally Nasoro Rufunga amekabidhi misaada hiyo kwa wenyeviti wa serikali za vitongoji na vijiji pamoja na kutoa fedha zaidi ya shilingi milioni nne kwa kaya 14 ambapo kila familia iliyofiwa imepatiwa kiasi cha shilingi laki tatu kama pole ya rambirambi ya serikali ya mkoa wa shinyanga na kuahidi kusaidia zaidi kadri misaada inavyopatikana.
Share To:
Magpress

MagPress

Vestibulum bibendum felis sit amet dolor auctor molestie. In dignissim eget nibh id dapibus. Fusce et suscipit orci. Aliquam sit amet urna lorem. Duis eu imperdiet nunc, non imperdiet libero.

0 comments so far,add yours