Rais Jakaya Kikwete afanya ziara ya kushtukiza katika eneo la Buguruni Mnyamani ili kujionea madhara makubwa ya mvua zinazoendelea kunyesha jijini Dar es salaam na kusababisha zaidi ya watu 1500 kukosa hifadhi baada ya nyumba zao kuingiwa na maji.
Baada ya Rais Kikwete kuwasili  katika eneo hilo la Buguruni Mnyamani jijini Dar es salaam huku akizingirwa na umati mkubwa wa watu,baadhi ya wakazi hao wamesikika wakipongeza ujio wa rais kufika katika eneo hilo ili kujionea walivyokimbia makazi yao baada ya maji  kuingia katika nyumba zao na kuwalazimu kulala nje wakilinda mali zao.
 
Akizungumza na wakazi wa Buguruni Mnyamani,Rais Kikwete amesema amelazimika kufika katika eneo hilo ili kuona jitihada zinazofanyika za kuondoa maji hayo ili wananchi wawe salama huku akikisisitiza kuwa baada ya maji hayo kuondolewa, ujenzi wa bomba mpya ambao ni mkubwa ufanyike ili kusaidia kupitisha maji wakati wa mafuriko.
 
Baadhi ya wakazi wa maeneo hayo akiwemo mzee Saidi Mohamed Bakari amesema wanaishi maisha ya tabu na wana siku saba hawajalala kutokana na maji hayo kuingia ndani ya nyumba zao.
Share To:
Magpress

MagPress

Vestibulum bibendum felis sit amet dolor auctor molestie. In dignissim eget nibh id dapibus. Fusce et suscipit orci. Aliquam sit amet urna lorem. Duis eu imperdiet nunc, non imperdiet libero.

0 comments so far,add yours