Bunge limechachamaa na kutaka 
serikali ianze kuchukua hatua kali za kisheria ikiwa ni pamoja na 
kuwakamata, kuwashtaki na kuwafilisi wale wote wanaohusika katika 
ubadhirifu na upotevu wa fedha za serikali kutokana na kukosa uzalendo 
na uwajibikaji badala ya kila mwaka bunge kupokea ripoti ya ubadhirifu 
unaosababishia taifa hasara ya mabilioni ya shilingi na kwamba kujiuzulu
 ama kufukuzwa kazi pekee si suluhisho ili kuwa na taifa lenye nidhamu 
katika matumizi ya fedha za umma.
Bunge limepata fursa ya kuzijadili taarifa za kamati ya bunge ya 
hesabu za serikali ambayo taarifa yake inaonesha kuwa zaidi ya shilingi 
bilioni 100 zimekwepwa kulipwa na makampuni mbalimbali kwa kivuli cha 
misamaha ya kodi na takribani bilioni 8 nazo zikipotea baada ya mamlaka 
ya bandari kufanya manunuzi ya dharura bila kibali cha mlipaji mkuu wa 
serikali jambo liliwafaanya baadhi ya wabunge kugeuka mbogo.
Hata hivyo wakati majadiliano yakiendelea kukaibuka mabishano ya 
kisheria dhidi ya mh Tundu Lissu na mwanasheria mkuu wa serikali Ndg 
George Mcheche Masaju baada Mh Lisu kutaka rais awawajibishe baadhi ya 
majaji waliohusika katika sakata la Tegeta Escrow kwa kuwa katiba inampa
 mamlaka huku ndg Masaju akiliambia bunge tume ya utumishi wa mahakama 
kwa mujibu wa katiba ndio inapaswa kumshauri rais juu ya masuala ya 
nidhamu za majaji.
Kutokana na kile kinachodaiwa kuwa ni kuepuka kuingilia mihimili 
mingine hasa mahakama baaadhi ya wabunge wameonesha kutoridhika na hoja 
hiyo kutokana na wabunge kuzuiwa kulijadili sakata la uda kutokana na 
taarifa za uwepo wa kesi kadha wa kadha mahakamani zinazohusu uda  baada
 ya mwanasheria mkuu wa serikali kushauri kutojadiliwa bungeni kutokana 
na kamati ya bunge ya hesabu za serikali za mitaa kuitaka serikali kutoa
 maelezo bungeni endapo ni kweli hisa za uda zimeuzwa kwa kampuni 
binafsi ya simon group limited ama la.
Mara baada ya muongozo huo mwenyekiti Mh Musa Azan Zungu akaitaka 
kamati uongozi ya bunge kukutana ili kulijadili suala hilo kwa madai 
kuwa kuna mambo yako mahakamani na mengine hayapo mahakamani lakini 
bunge linakosa fursa ya kuyajadili.

0 comments so far,add yours