Chama cha demokrasia wilayani Iringa kimelalamikia rafu na kasoro 
mbalimbali zilizojitokeza katika uchaguzi wa serikali za mitaa 
uliofanyika Disemba 14 nakusema kuwa uchaguzi huo uligubikwa na kasoro 
nyingi ambapo wakati uchaguzi huo ukiendelea hii leo watu wasiojulikana 
wamemshambulia kwa nondo na mapanga katibu wa mbunge wa Iringa mjini 
Bwana Joseph Mgima.
Akizungumza kwenye mahojiano na ITV Bwana Mgima amesema tukio hilo 
lilitokea usiku wa jana majira ya saa mbili usiku wakati alipokuwa 
akienda kuzungumza na mawakala wa chama chake kwenye mtaa wa Bwawani 
kata ya Mkwawa ndipo alipokutana na watu hao waliokuwa kwenye bajaji 
mbili ambapo mmoja wa watu hao alimpiga teke na kuangukia mtaroni ndipo 
watu wengine sita kutoka kwenye hizo bajaji walipoanza kumpiga kwa 
mapanga.
 
 
Akizungumza kwenye mahojiano na ITV Bwana Mgima amesema tukio hilo 
lilitokea usiku wa jana majira ya saa mbili usiku wakati alipokuwa 
akienda kuzungumza na mawakala wa chama chake kwenye mtaa wa Bwawani 
kata ya Mkwawa ndipo alipokutana na watu hao waliokuwa kwenye bajaji 
mbili ambapo mmoja wa watu hao alimpiga teke na kuangukia mtaroni ndipo 
watu wengine sita kutoka kwenye hizo bajaji walipoanza kumpiga kwa 
mapanga.
Mwenyekiti wa baraza la vijana la chaama cha demokrasia na 
maendeleo Chadema wilaya ya Iringa Leonce Marto amesema tukio hilo 
linauhusiano mkubwa na uchaguzi wa marudio wa wenye viti na wajumbe 
katika mitaa 19 katika manispaa ya Iringa akiwatuhumu wapinzani wao wa 
CCM kutumia mbinu chafu kushinda kwenye mitaa hiyo huku kamanda wa 
polisi mkoani Iringa Ramadhani Mungi akisema jeshi hilo linachunguza 
tukio hilo na litawashughulikia wote watakaobainika kufanya uhalifu huo.
Zoezi la uchaguzi linafanyika hii leo ikiwa ni marudio baada ya 
baadhi ya maeneo katika mitaa ya manispaa ya Iringa kushindwa kufanya 
uchaguzi huo kutokana na kasoro mbalimbali zilizojitokeza ikiwemo 
kukosekana kwa baadhi ya vifaa ambapo jumla ya mitaa 10 inarudia 
kuchagua wenyeviti wa mitaa na wajumbe wao na mitaa mingine 9 inarudia 
uchaguzi wa wajumbe baada ya wajumbe hao kugona kwa idadi ya kura.

0 comments so far,add yours