Chama cha mapinduzi CCM kimesema hakioni sababu ya suala la 
waliohusika kusababisha dosari zilizojitokeza wakati wa zoezi la upigaji
 kura kuundiwa tume au kuchunguzwa wakati wanajulikana, badala yake 
wachukuliwe hatua, huku kikieleza kusikitishwa na mapungufu 
yaliyojitokeza ambayo wamedai yalitokana na uzembe wa watendaji 
wachache.
Katibu wa itikadi na uenezi wa chama hicho Bw Nape Nnauye ameyasema
 hayo jijini Dar es Salaam ambapo amesema wakati umefika utaratibu wa 
kuunda tume kila jambo ufe kwani ni matumizi mabaya ya fedha na mwisho 
wa siku zinaleta ripoti machungungu ya jambo yakiwa yameisha hivyo 
haifanyiwi kazi tena huku akielezea namna CCM ilivyofanya vizuri katika 
uchaguzi wa serikali za mitaa.
Aidha kwa mara ya kwanza Bw Nape amevipongeza vyama vya upinzani 
kwa hatua vilivyofikia lakini akadai kuwa kwa umri waliofikia tangu 
vianzishwe hapa nchini havikupaswa kuwa hatua vilivyopo hivi sasa bali 
walitakiwa kuwa mbele zaidi huku akivitaka kutekeleza yale yote 
waliyoahidi kwa wananchi waliowapa dhamana na kuongeza kuwa furaha ya 
CCM ni kuona mfumo wa ushindi unakuwa.

0 comments so far,add yours