
Mmoja 
kati ya wafanyabiashara wakubwa wa nchini Marekani mwenye asili ya 
Afrika Dr.Robert Shumake amekubali kuzileta treni za kisasa katika jiji 
la Dar es salaam ili kusaidia kutatua kero ya usafiri katika jiji hilo 
ambapo anatarajia kutumia zaidi ya shilingi Bilioni arobaini kufanikisha
 hilo muda wowote kuanzia sasa.
 
 
Akizungumza mara baada ya kutia saini makubaliano ya uletaji wa 
treni hizo Dr.Shumake amesema anatarajia treni hizo zitafanya kazi saa 
ishirini na nne na anaisubiri serikali ya Tanzania imalize tathmini ya 
gharama za mradi huo na yeye aweze kutoa fedha za kuufanikisha.
Naye waziri wa uchukuzi Dr.Harrison Mwakyembe amesema treni hizo 
zitafanya kazi kati ya Stesheni na Pugu na zitatumia miundombinu ya reli
 iliyopo ila kutakuwa na ujenzi wa reli zingine katika baadhi ya sehemu 
kuruhusu treni kupishana.

0 comments so far,add yours