Mfanyabiashara wa Tanzania Bw. Patrick Ngowi ni miongoni mwa 
wafanyabiashara 100 walioingia fainali za kuwania tuzo ya mfanyabiashara
 bora kijana wa mwaka barani afrika, zitakazofanyika Afrika kusini 
novemba 14 mwaka huu.
Akiwa na umri wa miaka 28, Bw. Patrick Ngowi ambaye ni mwenyekiti 
wa kampuni ya Helvetic Group, inayotengeneza vifaa vya umeme wa jua, 
ametangazwa kuwa ni miongoni mwa wafanyabiashara 100 walio na umri 
usiozidi miaka 40, waliofanikiwa na wanaotarajiwa kufanya vizuri zaidi 
miaka ijayo.
Katika orodha hiyo wapo watanzania wengine 9, ikiashiria kuwa kuna 
uwezekano kuwa asilimia 10 ya wafanyabiashara wakubwa wa miaka ijayo 
barani Afrika, watakuwa ni watanzania.
Kwa mujibu wa rais wa taasisi ya Choiseul Bw. Pascal Larot, kila 
mwaka taasisi yake hufanya utafiti wa kusaka na kuorodhesha katika 
madaraja wafanyabiashara vijana wanaochipukia kiuchumi, wenye umri 
usiozidi miaka 40, ambao watashiriki kikamilifu katika kujenga uchumi wa
 bara hili miaka ya hivi karibuni.
Hivi karibuni chaneli ya televisheni ya mambo ya fedha na biashara -
 CNBC ilimtunuku Bw. Patrick Ngowi tuzo ya mwaka ya mfanyabiashara 
kijana wa Afrika Mashariki, katika hafla iliyofanyika jijini nairobi, 
kenya, ambayo mwenyekiti mtendaji wa IPP Dr Reginald Mengi pia 
alitunukiwa  tuzo ya mfanyabiashara bora wa mwaka Afrika Mashariki.

0 comments so far,add yours