Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samia Suluhu amewataka viongozi wa siasa na serikali kufuata taratibu za uwajibishwaji wa watumishi pindi inapotokea kasoro katika utendaji wao.
Akizungumza na Wauguzi na wananchi wa mkoa wa Geita katika siku ya wauguzi duniania ambapo kitaifa imefanyika katika mkoa wa Geita Mama Samia amesema serikali itaendelea kuboresha stahiki na mazingira ya kazi kila itakapoweza ili kuwafanya watumishi wa umma kufanya kazi katika mazingira bora.

Naye Waziri wa Tawala za mikoa na serikali za mitaa Mheshimiwa George Simbachawene amesema atasimamia na kuhakikisha haki za wauguzi zinapatikana kwa wakati ili kuboresha huduma ya afya nchini.

Awali akisoma risala mbele ya mgeni rasmi Rais wa chama cha wauguzi Tanzania Paul Magesa amesema mpaka sasa kuna uhaba wa wauguzi kwa asilimia hamsini na moja tu jambo hili huwafanya wauguzi kufanyakazi nyingi katika mazingira magumu hivyo kuomba ajira ziongezwe katika sekta hiyo.
Share To:
Magpress

MagPress

Vestibulum bibendum felis sit amet dolor auctor molestie. In dignissim eget nibh id dapibus. Fusce et suscipit orci. Aliquam sit amet urna lorem. Duis eu imperdiet nunc, non imperdiet libero.

0 comments so far,add yours