Waziri mpya wa Ujenzi, Mawasilaino na usafirishaji wa Zanzibar Balozi Ali Abeid Karume amewatahadharisha wafanyakazi wa wizara hiyo kuweka siasa pembeni na kuchapa kazi huku akiahidi hatofanya kazi kwa fitna na majungu na kuangalia itikadi za chama.
Balozi Karume ametoa tahadhari hiyo wakati wa makabidhiano ya wizara hiyo kutoka kwa waziri wa mwanzo wa awamu iliyopita  ambapo amesema huu si wakati wa kuhoji mfanyakazi anatoka chama gani ndipo apewe huduma ila ni wakati wa kuwatumikia wananchi na kuwapa huduma muhimu zote za kijamii zinazotokana na wizara hiyo ambayo inagusa hisia za watu wa rika zote.
Akizungumzia utendaji wa wizara Balozi Ali Karume amesema yeye ni mchapakazi ambaye anapenda kuwasikiliza wale anaofanyakazi nao na kuonya hatovumulia, mambo ya fitna na majungu ila anataka ushirikiano, kwa upande wake aliyekuwa naibu waziri wa wizara hiyo ya Mawasiliano Issa Haji ambaye alikabidhi kutokana na wizara hiyo kutokuwa na waziri baada ya kujiuzulu kwa Mhe Juma Duni amesema ana imani kuwa wizara hiyo mpya imepata mtaalamu na msomi na mwenye ujuzi wa kuendeleza wizara hyo.
Kikosi hicho kipya cha mawaziri wa Dr Shein mawaziri wake wamekuwa wakianza kwa kishindo na kutahadharisha kuwa huu si wakati wa siasa tena ila ni wa kuchapa kazi.
Share To:
Magpress

MagPress

Vestibulum bibendum felis sit amet dolor auctor molestie. In dignissim eget nibh id dapibus. Fusce et suscipit orci. Aliquam sit amet urna lorem. Duis eu imperdiet nunc, non imperdiet libero.

0 comments so far,add yours