Rais Jakaya Kikwete amevitaka vyombo 
vya upelelezi kutokukurupuka kwa kupeleka kesi mahakamani ambazo 
upelelezi haujakamailika matokeo yake wanashindwa kesi na kwamba huko ni
 kumnyima mtu haki kwa kupeleka mashitaka yasiyostahili.
 
 
Katika hotuba yake mwanasheria mkuu wa serikali Bw George Masaju 
amesema mahakama ndiyo kimbilio la watu wanaohitaji haki hivyo ina 
wajibu wa kuwasikiliza watu wanaofungua au kufunguliwa mashauri na kutoa
 uamuzi kwa kutenda haki kwa wote bila kujali hali ya mtu kijamii au 
kiuchumi, kutochelewesha haki, kutoa fidia ipasayo kwa watu 
wanaoathirika kutokana na makosa ya watu wengine.
 
Rais Kikwete ametoa rai hiyo jijini Dar es salaam wakati wa 
maadhimisho ya siku ya sheria nchini ambapo amesema watanzania lazima 
wapate haki tena kwa wakati na kuwataka mawakili, waendesha mashitaka na
 vyombo vya upelelezi kufanyakazi kwa pamoja ili visiwe chanzo cha 
kuchelewesha mashauri pasipo sababu na kama shitaka halikamilika 
wasikamate watu huku akielezea hatua mbalimbali serikali ilizochukuwa 
katika kuboresha mfumo wa mahakama.
Jaji mkuu wa Tanzania Mh Mohamed Chande Othuman amebainisha baadhi 
ya vikwazo vinavyochangia kukwamisha ufanikishwaji wa fursa ya wananchi 
kupata haki kuwa ni pamoja na sheria nyingi kutokuwa kwenye lugha ya 
taifa kwani zimeandikwa kwa lugha ya kiingereza, huku akilitaka bunge 
kuangalia namna ya kufanya ili sheria ziwe rafiki kwa watumiaji wote 
kwani watanzania wengi wanakosa haki kwa kutokuelewa lugha inayotumika.
Katika hotuba yake mwanasheria mkuu wa serikali Bw George Masaju 
amesema mahakama ndiyo kimbilio la watu wanaohitaji haki hivyo ina 
wajibu wa kuwasikiliza watu wanaofungua au kufunguliwa mashauri na kutoa
 uamuzi kwa kutenda haki kwa wote bila kujali hali ya mtu kijamii au 
kiuchumi, kutochelewesha haki, kutoa fidia ipasayo kwa watu 
wanaoathirika kutokana na makosa ya watu wengine.
Akisoma hotuba ya chama cha wanasheria Tanganyika TLS rais wa chama
 hicho Charles Rwechungura amesema uelewa mdogo wa sheria miongoni mwa 
wananchi unachangia kuzuia upatikanaji wa haki ambapo ametolea mfano 
mkoa wa Dodoma ambako wamebaini kuwa idadi kubwa ya watu walipoteza haki
 zao za umiliki wa ardhi na masuala ya ndoa kwa sababu ya kutokujua njia
 gani watumie ili kupata haki hadi muda wa ukomo uliowekwa chini ya 
sheria ulipomalizika.

0 comments so far,add yours