Spika wa bunge Mh Anna Makinda amesema siyo jukumu lake kuwaondoa 
wenyeviti wa kamati za bunge ambao wanatuhumiwa katika sakata la akaunti
 ya Tegeta Escrow isipokuwa wao wenyewe wanatakiwa kutii azimio la bunge
 namba tatu linalowataka wajiuzulu.
Wakati Mh Makinda akieleza hayo tena kwa kusisitiza kuwa wenyeviti 
hao tayari wameshajiuzulu baadhi ya kamati ikiwemo ya katiba na sheria 
ambayo mwenyekiti wake ni Mh William Ngeleja ambaye ni miongoni mwa 
wabunge wanaotuhumiwa kwenye sakata hilo bado anaendelea na wadhifa huo.
Mh Makinda ametoa ufafanuzi huo wakati akijibu maswali ya waandishi
 wa habari mara baada ya kupokea msaada wa vifaa vya Teknohama 
vilivyotolewa na serikali ya China kupitia balozi wake hapa nchini 
ambapo amesema vifaa hivyo vitaweza kuokoa zaidi ya bilioni moja ambazo 
hutumika kuchapisha miswada mbalimbali na taarifa nyingine za bunge 
badala yake sasa wabunge watakuwa wanatumiwa moja kwa moja kwenye 
mtandao.
Akikabidhi vifaa hivyo vyenye thamani ya dola za kimarekani laki 
moja balozi wa china hapa nchini Lu Youqing amesema vifaa hivyo ni ahadi
 aliyoitoa rais wa China wakati wa ziara yake hapa nchini ambapo 
alimwahidi spika wa bunge Mh Makinda na kuongeza kuwa china imewekeza 
zaidi ya dola bilioni 3.1 hasa sekta ya kilimo na viwanda na kwamba kuna
 kampuni zaidi ya 500 zinazomilikiwa na wachina ambazo zimetoa ajira kwa
 watanzania laki moja.

0 comments so far,add yours