Taasisi ya Sekta Binafsi nchini -TPSF imeanzisha Mfuko Maalum wa kuwawezesha wanawake kugombea ubunge wa kuchaguliwa.
 
Akizungumza katika mkutano huo Mbunge wa Hanang, ambaye pia ni 
Waziri wa Nchi ofisi ya Waziri Mkuu, Uwekezaji na Uwezeshaji Dr. Mary 
Nagu amesema wanawake hawana budi kuwania nafasi za ubunge wa 
kuchaguliwa, na kusisitiza kuwa ili  harakati zao zifanikiwe ni lazima 
ziungwe mkono na wanaume.
 
 
 
Uanzishwaji wa mfuko huo jijini Dar es salaam ni matokeo ya Mkutano
 wa pamoja wa mashauriano baina ya TPSF na Wabunge Wanawake Wenye 
majimbo nchini, uliokusudia kutafuta namna ya kuwawezesha wabunge 
wanawake kushiriki na kushinda majimbo katika uchaguzi mkuu ujao.
Akizungumza katika mkutano huo Mbunge wa Hanang, ambaye pia ni 
Waziri wa Nchi ofisi ya Waziri Mkuu, Uwekezaji na Uwezeshaji Dr. Mary 
Nagu amesema wanawake hawana budi kuwania nafasi za ubunge wa 
kuchaguliwa, na kusisitiza kuwa ili  harakati zao zifanikiwe ni lazima 
ziungwe mkono na wanaume.
Mapema Mwenyekiti wa TPSF Dr. Reginald Mengi aliwahamasisha 
wanawake nchini kujiamini kuwa wanaweza kufanya makubwa, iwapo harakati 
zao za kupigania usawa zitawashirikisha pia wanaume.
Kuhusu Mfuko huo Dr Mengi amesema mtaji wake wa kuanzia utakuwa wa 
kiasi cha shilingi milioni 100, ambapo jumla ya shilingi milioni 19.5 
ziliahidiwa kuchangwa na wanachama wa TPSF waliohudhuria mkutano huo.
Wakati wa mkutano huo Baadhi ya wabunge wanawake na wanachama wa 
TPSF waliotoa maoni mbalimbali kuhusu namna ya kuendeleza ushirikiano 
baina yao.

0 comments so far,add yours