Kamati ya kudumu ya Bunge ya hesabu za serikali imependekeza 
kufukuzwa kazi kwa waziri wa nishati na madini kutokana na kulipotosha 
bunge na taifa kwa ujumla kuhusiana na fedha ya akaunti ya Tegeta Escrow
 pamoja na kuwa dalali mkuu aliyewakutanisha Bwana Harbinder Sigh Sing 
Set na Bwaba Rugemalila katika ofisi za umma.
 
Kamati imependekeza waziri mkuu Mheshimiwa Mizengo Pinda kuwajibika
 kutokana na kauli zake za kuaminisha umma kuwa fedha zile siyo za umma 
kiasi kwamba vyombo vya habari ikiwemo gazeti la Daily News kuchapisha 
habari yenye kichwa cha habari kilichoandika hakukuwa na tatizo katika 
IPTL kauli inayoonyesha alishindwa kutekeleza wajibu wake.
 
 
Akiwasilisha taarifa ya kamati kufuatia matokeo ya ukaguzi maalumu 
wa mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali katika akauti ya 
Tegeta Escrow amesema waziri wa nishati na madini alifanya udalali huo 
akijua dhahiri kuwa Bwana Sethi hana uhalali wa kisheria kufanya 
biashara kwa jina la IPTL.
Kamati imependekeza waziri mkuu Mheshimiwa Mizengo Pinda kuwajibika
 kutokana na kauli zake za kuaminisha umma kuwa fedha zile siyo za umma 
kiasi kwamba vyombo vya habari ikiwemo gazeti la Daily News kuchapisha 
habari yenye kichwa cha habari kilichoandika hakukuwa na tatizo katika 
IPTL kauli inayoonyesha alishindwa kutekeleza wajibu wake.
Aidha mwenyekiti wa PAC Bwana Zitto Kabwe amesema kamati hiyo 
inapendekeza mwanasheria mkuu wa serikali uteuzi wake utenguliwe na 
afikishwe mahakamani kwa matumizi mabaya ya ofisi yaliyopelekea serikali
 mabilioni ya shilingi. 
Taja majina ya viongozi waliopata mgao wa fedha za Tegeta Escrow 
wakiwemo viongozi wa dini na baadhi ya watumishi wa idara na taasisi za 
serikali.

0 comments so far,add yours