JKT huandikisha vijana wa kujitolea 
kutoka mikoa yote ya hapa nchini kila mwaka. Utaratibu unaotumika ni kwa
 JKT kuandika barua kwa wakuu wa Mikoa na kuanisha nafasi ambazo mkoa 
umetengewa.
Baada ya Mkoa kupata barua kutoka kwa 
Mkuu wa JKT na idadi ya nafasi za vijana waliopangiwa kujiunga. Mkoa 
hugawa nafasi hizo kulingana na wilaya zake. Pia wilaya zinatakiwa 
kupeleka katika tarafa, kata na vijiji. Mara nyingi uongozi wa wilaya 
hubandika tangazo la nafasi hizo katika ubao wao wa matangazo. JKT 
hutangaza nafasi za kujiunga na jeshi hilo kupitia vyombo vya habari vya
 Serikali na biafsi kwa nia ya kuharakisha taarifa kuwa. kia wananchi 
hasa vijana. Usaili wa awali hufanyika chini ya Kamati za Ulinzi na 
Usalama za Wilaya wanakotoka vijana hao, baadaye hufanyika mkoani, ili 
kupata idadi ya vijana wa mkoa mzima.
Zoezi hilo linapokamilika mikoani, JKT 
hutuma timu za maafisa na askari kutoka Makao Makuu ya JKT kwa ajili ya 
kuhakiki vijana waliosailiwa katika mikoa yote ya Tanzania Bara. Vijana 
hupimwa afya zao na kusafirishwa katika vikosi vya JKT.
Kabla ya kuondoka timu za usaili kutoka 
JKT hufanyiwa semina na kuelekezwa jinsi ya kubaini udanganyifu wa vyeti
 bandia vya kuzaliwa na shule. Mhariri Mkuu wa Jarida la Vijana Leo 
alikuwa ni miongoni mwa watu walioshiriki usaili mkoani Ruvuma. Vijana 
wa mkoa huo walitoka katika Wilaya za Songea Mjini, Vijijini, Namtumbo, 
Mbinga na Tunduru na kukusanyika Makao Makuu ya Mkoa wa Ruvuma. Vijana 
hao walikuwa na shauku ya kupata nafasi ya kujiunga na JKT.

0 comments so far,add yours