
Mratibu
 wa matembezi hayo Bw, Matukio Chuma akiongea na waandishi wa habari 
kwenye ukumbi wa Idara ya habari (MAELEZO), jijini Dar es Salaam wakati 
akizindua  matembezi yajulikanayo kama, Matembezi ya Nchi Yangu Wajibu 
Wangu, yanayo tarajiwa kuanza, Januari 11-2014 kuanzia jijini Dar es 
Salaam hadi Mkoani Morogoro matenzi hayo ya kilomita (200km), ambayo 
yatachukua siku kumi 10,lengo la matembezi hayo kuhamasisha kila 
Mtanzania kuamua kuchukua hatua kujikwamua kimaisha.
 Ni
 changamoto inayotolewa mbele ya Watanzania,kukumbuka maana halisi ya  
uzalendo kujitoa mhanga kuweza kufanyikisha maendeleo yao wenyewe kwa 
kujishughulisha na kujibidisha katika Nyaja mbalimbali kwa manufaa ya 
Taifa,kujitolea kuanzia ngazi ya kaya mpaka taifa,kuacha kulalama tu 
kuwa serikali haijawafanyia moja ama mbili lakini wao wenyewe kutambua 
mchango wao kama Watanzania na wajibu wao kama wananchi, kubwa zaidi 
kujivunia nchi iitwayo Tanzania kwa yale mema na adimu yaliyopo na 
kurekebisha palipo na kasoro kwa moyo mmoja bila kujali itikadi,imani, 
asili ama mtizamo miongoni mwetu, Tanzania,kwa nini Dar es Salaam mpaka 
Morogoro.Dar es Salaam imendelea kuwa kituo kikuu cha shughuli nyingi za
 kiuchumi, kiserikali na vilevile ni mkoa ulio na watu wengi zaidi 
Tanzania, ta kribani milioni mbili na nusu (2.5mil) kawa mujibu wa sensa
 ya watu ya mwaka 2002, wakati Morogoro ina watu wasiofika laki tatu tu,
 na kwa ukuaji wa asilia 4.39 kawa mwaka inaweka pia kuwa ya watu barani
 Afrika na tisa duniani, hii inawakilisha tofauti kubwa sio tu kwa idadi
 lakini ya ukuaji, upatikanaji wa huduma za msingi za kijamii, ukuaji wa
 kiuchumi na vilivile hali ya kipato na fursa za iuchumi” alisema Chuma.
Mratibu
 wa matembezi hayo Bw. Matukio Chuma akiwaonyesha waandshi wa habari 
vazi litakalotumika kwenye matembezi hayo (kushoto), Mratibu wa 
matembezi hayo Carren Mgonja.
Waandishi wa habari wakishuhudia uzinduzi huo.(PICHA NA PHILEMON SOLOMON WA FULLSHANGWE DAR ES SALAAM).



0 comments so far,add yours