Shrikisho
 la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limepokea kwa masikitiko kifo cha 
mchezaji wa zamani wa timu za Coastal Union, TPC na Taifa Stars, Behewa 
Ali Sembwana (72) kilichotokea jana usiku (Machi 31 mwaka huu) mkoani 
Tanga.
Msiba
 huo ni mkubwa kwa wadau wa mpira wa miguu kwani kwa nyakati tofauti 
Sembwana akiwa mchezaji, alitoa mchango mkubwa kwa timu mbalimbali 
alizochezea, hivyo mchango wake tutaukumbuka daima.
Sembwana
 aliyekuwa akicheza wingi ya kulia alidumu katika Taifa Stars kwa miaka 
kumi, kama ilivyokuwa kwa kombaini ya Mkoa wa Tanga (Tanga Stars) 
aliyoiwakilisha katika michuano ya Kombe la Taifa (Taifa Cup).
TFF
 inatoa pole kwa familia ya marehemu Sembwana, Chama cha Mpira wa Miguu 
Mkoa wa Tanga (TRFA) na klabu ya Coastal Union na kuwataka kuwa na 
subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha msiba huo mzito.
Maziko
 yanatarajiwa kufanyika leo (Aprili 1 mwaka huu) kijijini kwake Lusanga,
 Wilaya ya Muheza mkoani Tanga. Mungu aiweke roho ya marehemu Sembwana 
mahali pema peponi. Amina
MECHI
 ya marudiano ya raundi ya kwanza ya Kombe la Shirikisho kati ya Azam ya
 Tanzania na Barrack Young Controllers II ya Liberia iliyochezwa jana 
(Aprili 6 mwaka huu) imeingiza sh. 44,229,000.
Fedha
 hizo katika mechi hiyo iliyochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na 
kumalizika kwa timu hizo kutoka suluhu zimetokana na watazamaji 17,128 
waliokata tiketi.
Viingilio
 vilikuwa sh. 2,000, sh. 5,000, sh. 10,000 na sh. 20,000 ambacho 
kilikuwa kiingilio cha juu kwa jukwaa la VIP A. Kiingilio cha sh. 2,000 
ndicho kilichovutia watazamaji wengi ambapo walikuwa 15,212.
Mgawo
 ulikuwa kama ifuatavyo; gharama za tiketi sh. 5,575,500, asilimia 15 ya
 uwanja sh. 5,798,025, asilimia 10 ya Shirikisho la Mpira wa Miguu 
Tanzania (TFF) na Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) sh. 
3,865,350 na asilimia 75 iliyokwenda kwa klabu ya Azam ni sh. 
28,990,500.
Mechi
 iliyopita ya raundi ya awali ya mashindano hayo kati ya Azam na El 
Nasir ya Sudan Kusini iliyochezwa kwenye uwanja huo huo Februari 16 
mwaka huu iliingiza sh. 34,046,000 kwa viingilio hivyo hivyo huku 
ikishuhudiwa na watazamaji 13,431.
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

                    
				
0 comments so far,add yours