Arusha. Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa ameshangazwa na polisi kuhusu uzuiwaji wa mikutano ya kisiasa akisisitiza kuwa ni kinyume cha sheria.
Kutokana na hali hiyo, ameibuka na mkakati mpya wa kuhutubia wananchi kwa kutumia mitandao ya kijamii. “Kuzuia mikutano ya kisiasa ni kwenda kinyume na sheria. Sheria imeruhusu mikutano yote ya kisiasa. Lakini hawawezi kutuzuia, sisi tutafanya mikutano na kuhutubia kwa kutumia mitandao ya kijamii na tutawapa wananchi fursa ya kuuliza maswali na tutayajibu,” amesema jana katika mkutano wa mameya na wenyeviti wa halmashauri zilizo chini ya Chadema jijini hapa. #mwananchi
Share To:
Magpress

MagPress

Vestibulum bibendum felis sit amet dolor auctor molestie. In dignissim eget nibh id dapibus. Fusce et suscipit orci. Aliquam sit amet urna lorem. Duis eu imperdiet nunc, non imperdiet libero.

0 comments so far,add yours