Wananchi wa Wilaya ya Meatu Mkoani Simiyu wamemuomba Waziri Mkuu ,KASIM MAJALIWA kuwasaidia kuondoa mgogoro uliopo kati yao na mwekezaji wa kampuni ya Mwiba Holidings ambaye amekuwa akiwakamata wananchi  na kuwapiga jambo walilosema  ni unyanyasaji.
Akizungumza kwa niaba ya wananchi hao Mbunge wa jimbo hilo,SALUM KHAMIS  amemw ambia Waziri Mkuu kuwa mwekezaji hu y o amekuwa kero kubwa kwa wananchi wa Meatu  hasa wanaoishi   kando kando ya Pori la Akiba la Makao.
Mbunge huyo pia amemuomba Waziri Mkuu kupitia upya mikataba ya mwekezaji huyo ambayo amesema imejaa utapeli mwingi  na kwamba wananchi wa Meatu wamechoshwa na uonevu huo .
Akijibu malalalmiko ya wananchi hao katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya Stendi Mwanhuzi Waziri Mkuu,KASIM MAJALIWA amesema Serikali tayari kuwavumilia wawekezaji  wanaonyanyasa wananchi .
Waziri mkuu amemuagiza Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,ELASTON MBWILO akutane na mwekezaji hiyo na ifikapo tarehe 11 mwezi huu ampe taarifa na kama itaonekana ni jipu basi litatumbuliwa.

Share To:
Magpress

MagPress

Vestibulum bibendum felis sit amet dolor auctor molestie. In dignissim eget nibh id dapibus. Fusce et suscipit orci. Aliquam sit amet urna lorem. Duis eu imperdiet nunc, non imperdiet libero.

0 comments so far,add yours