Jeshi la polisi mkoani Mara limezima  maandamano ambayo  yameitishwa na Chama cha demokrasia na  maendeleo Chadema  wilayani Bunda  mkoani Mara,huku viongozi  kadhaa  wa  chama  hicho   wakikamatwa na jeshi  la  polisi  kwa  madai  ya  kukaidi  amri halali ya jeshi hilo.
Askari wa jeshi la polisi wakiwemo wa kikosi cha kutuliza ghasia wa FFU wakiwa  katika  magari manne  tofauti walianza  kufika katika mji wa Nyasura wilayani Bunda eneo ambalo lilipangwa na Chadema  kunzia maandamano hayo, kisha  kutolewa  kwa  amri   ambayo  iliwataka  wafuasi hao wakiwa na mabango yenye ujumbe mbalimbali kutawanyika mara moja katika eneo hilo.
Hata  hivyo  baada  ya  baadhi  ya  wafuasi  na    viongozi  hao   wa  Chadema  kukaidi   amri  hiyo, polisi  walianza  kurusha  mabomu  ya  machozi  kisha kuwakamata watu  kadhaa  wakiwemo viongozi  chama  hicho   wilaya  ya Bunda.
 wakizungumzia hali hiyo  baadhi  ya viongozi  wa chadema  wilaya ya bunda,wamelalamikiwa  hatua ya  jeshi la polisi  kutumia  nguvu  kubwa kuzima maandamano hayo  ambayo  wameyaita  kuwa ya  amani.
Naye  kamanda wa polisi mkoani Mara ACP Philip Alex Kalangi,akizungumza kwa njia ya simu amesema jeshi la polisi limewakamata watu kumi  wakiwemo viongozi  wa chama hicho  wilayani Bunda  kwa kushindwa  kutekeleza agizo  la jeshi  hilo  lilowata kusitisha  maandamano hayo  ya  kupinga  kuendelea  kwa bunge  la  katiba  ambalo amesema  linaendeshwa kwa  mujibu  wa  sheria.
Share To:
Magpress

MagPress

Vestibulum bibendum felis sit amet dolor auctor molestie. In dignissim eget nibh id dapibus. Fusce et suscipit orci. Aliquam sit amet urna lorem. Duis eu imperdiet nunc, non imperdiet libero.

0 comments so far,add yours